TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Saturday, October 13, 2012

SAKATA LA WAISLAMU MBAGALA...

Vurugu zilizofuatia mtoto aitwae Emmanuel Josephat (14), Kukuojolea msahafu (Quran) zimechukua sura mpya baada ya baadhia ya waumini wa dini ya kiislam kukusanyika na kushinikiza mtoto huyo aachiwe na polisi ili wamuue.
Waumini hao wanaokadiriwa kifikia idadi ya watu 3000 baada ya kutawanywa na polisi waliingia mitaani na kuchoma moto kanisa la kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Mbagala Zakhem, wakaharibu Kanisa la Anglican, wakavunja vioo vya kanisa la wasabato, na kuchoma moto Tanzania Assembly Of God (TAG) la mbagala Mbagala kizuiani na kuchukua vifaa vya muziki vya kanisa hilo...
Awali waumini hao walikusanyika katika kituo hicho cha polisi cha maturubai, Mbagala kizuiani wakitaka mtoto huyo ambaye alikuwa nchini ya ulizi wa polisi aachiwe, na polisi walipokataa matakwa yao ndipo vurugu hizo zilipoanza.
Chanzo cha Tukio hili ni mabishano baina ya watoto wawili, Emmanuel Josephat, na mtoto mwingine wa kiislam, kwa jina hatujalifahamu 


  Hamisi Salum, Baba wa mtoto ambaye amekojelewa Quran Yake, akiongea na vyombo vya habari
                                    Jeshi La FFU wakiwa wanajaribu kutuliza Fujo
                        Mmoja wa waandamaji akiwa amekamatwa na FFU
      Hawa Ndio Baadhi ya waandamaji waliokamatwa wakiwa wanapandishwa kwenye Gari ya polisi
               Baadhi ya watuhumiwa wakiwa wamekamatwa na Polisi
   Polisi wa Jeshi la FFU wakiwa katika harakati za kutuliza fujo za waandamanaji





        Moja ya Gari la Raia lililo haribiwa
              
          Mmoja ya kanisa yaliyo haribiwa huko mbagala

No comments:

Post a Comment